Taharuki juu ya audio inayosambaa kwenye social media ni kwamba Watanzania wanaporudi nchini Tanzania wanaporwa passport na mali na kufunguliwa kesi.
Ifatayo ni hiyo audio na chini yake ni majibu ya kukanusha kilichoongelewa kutoka kwa idara ya Uhamiaji, nchini Tanzania.
Pia kumekua na lawama kuwa nchi ya Tanzania inawaadhibu Watz wanaoamua kuhamia nchi nyingine kwa ajiri ya kutafuta maisha bora hasa pale uchumi wa Tanzania unaposhindwa kutoa fursa tosherezi. Watz wanaolazimika kuchukua uraia wa nchi nyingine ili kutii sheria za nchi walizomo wanadaiwa kuwa wamepoteza uraia wao wa kuzaliwa bila kupewa nafasi ya kusikilizwa mahakani. Inaelekea serikali ya Tanzania inaona ni bora raia wao wavunje sheria ya nchi walizomo kuliko kutafuta namna ya kuishi kwa misingi ya kisheria. Hapo hapo, kulingana na matukio yanayodaiwa kuendelea nchini Tanzania, watanzania wanalazimishwa kudhihirisha upanikanaji wa pesa wanazorudi nazo nchini mwao. Kwa lugha nyingine na kwa usalama zaidi mtanzania mtiifu ni kutosafiri nje ya nchi ama kurudi nchini bila kuwa na senti yoyote mfukoni. Ni kwa nini mtanzania aadhibiwe kwa kuchagua kuishi kwenye taifa lingine ama kurudi na alichokipata ng’ambo nchini Tanzania?
Ukanushaji, kutoka idara ya uhamiaji nchini Tanzania unasomeka kama ifatavyo:

