By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
LiwalonaliweLiwalonaliwe
  • Uvumi
  • Za Kitaa/Street Talks
  • Kijiweni
  • Dating
  • Career
Search
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Reading: Ninawaza kwa sauti!!
Share
Sign In
Notification Show More
Latest News
Kipi Bora: Mira ama taratibu za kidini
Kijiweni
Kuporwa Passport Tanzania
Uvumi
Inatosha!!
Za Kitaa/Street Talks
DC Ngara Katika Hili Umechemka, Kama ni Kweli Waombe Radhi Vijana
Uvumi
Ukimya ni Uoga ama ni Usalama?
Uvumi
Aa
LiwalonaliweLiwalonaliwe
Aa
Search
  • Uvumi
  • Za Kitaa/Street Talks
  • Focused Affairs
    • Dating
    • Career
    • Kijiweni
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Liwalonaliwe > Kijiweni > Ninawaza kwa sauti!!
Kijiweni

Ninawaza kwa sauti!!

Mzee
Last updated: 2025/09/07 at 9:57 PM
Mzee
Share
Mchungaji Gwajima na mbunge wa Kawe
SHARE

Na Sam Ruhuza

Askofu Gwajima aliita press conference kama Mtanzania na kuongelea suala la Utekaji na kulaani pakubwa watekaji na kuonyesha kuumia sana na hali hiyo hadi kuwatolea mfano watoto wa wakuu akiwamo mkuu kabisa, akihoji iwapo wangevumilia watu wasiojulikana kuendelea kuteka?! 

Kilichofuata baada ya kauli yake; 

– Wabunge wenzake wa chama chake, badala ya kujadili bajeti ya Wizara ya Ndani, wao wakaishia kumjadili Gwajima na kulaani mfano wake wa kuteka mtoto wa Mkuu! Wengine tuliona ujumbe umefika maana waliumia na ndio ilikuwa nia ya mfano huo, zaidi ya maneno yao ilikuwa uchawa tu majina yao yapitishwe kwenye uchaguzi ndani ya chama!! 

– Mkiti wa chama chake kwenye mkutano mkuu aliwataka wanachama kuwaacha wakina Gwajima,  yaani wenye mawazo kama ya Gwajima na kuwaita Gwajimanized chama! 

– Ubunge wake ndipo ulipoishia hapo! 

– Alipotangaza kufunga na kusali kwa Makanisa anayoyaongoza kwa ajili ya kuliombea Taifa lipone dhidi ya Utekaji, kesho yake Kanisa yaani Dhehebu lake nchi nzima likafutwa kwa Msajili! 

– Tukaanza kuona kwenye videos Waumini wa Kanisa lake wakaanza kushambuliwa kwa marungu na Police kila walipokwenda Kanisani kuabudu! 

Hadi leo hatujasikia Kanisa au Dhehebu hilo likifunguliwa!! 

Naendelea kuwaza kwa sauti, leo chama cha siasa chadema tumewasikia wakienda kufariji familia za waliotekwa na wengine kuamua kwenda Kanisani kuabudu na kumuomba Mungu, inaelezwa Police wamewavamia Kanisani wakiwa kwenye sala na kuwachukua!!! 

Nawaza kwa sauti huku nikikosa majibu, kwanini anayeongelea au kuombea utekaji ukome, anapata mtihani na Police, Kulikoni?! 

Kwanini haya yanatokea Kanisani kwenye Ibada?! 

Ninawaza, Je ni majibu ya Mungu kuonyesha watekaji?! 

Kwanini Wabunge walimlaani sana Mbunge mwenzao Gwajima kwa hoja yake badala ya angalau kujadiliana Utekaji, mbona Mheshimiwa Rais alipoongelea kutopendezewa na hali ya Utekaji na kuwataka Police kuchukua hatua, haohao Wabunge walishangalia, nini tofauti yake??!! 

Nawaza kwa sauti, chama tawala kilipoambiwa kujitenga na wakina Gwajima na wajumbe kushangilia, walielewa nini??!! Au Mkiti wao alimaanisha nini??!!  

Je, kwa Mwananchi kuongelea Utekaji au kumuomba Mungu akomeshe hili ni kosa la jinai?! Inabidi tuambiwe ili tuelewe! 

Je, Chadema kuwa na matukio mengi ya kukamatwa kamatwa makosa yao ni nini ili tuelewe,  labda mtu kuwa chadema ni makosa?! 

Nawaza kwa sauti mfumo wa vyama vingi vya siasa ulivyoanza na kuendelea, japo ulikuwa mgeni na mapungufu yalikuwapo, lakini watu waliongea na kufurahi pamoja, hii watu wasiojulikana walipoanza kazi zao, hali imekuwa sio sawa, ni kuogopana na kuhisi mmoja ana haki zaidi ya mwingine! 

Kanisha la Ufufuo na Uzima la Josephat Gwajima lililopo Ubungo.

Taifa linapona kwa mijadala. 

Muhimu Tupendane na kuheshimu mawazo ya mwingine hata kama huyapendi! 

Tanzania ni yetu sote! 🇹🇿🤝💪

Sign Up For Daily Newsletter

Be keep up! Get the latest breaking news delivered straight to your inbox.
[mc4wp_form]
By signing up, you agree to our Terms of Use and acknowledge the data practices in our Privacy Policy. You may unsubscribe at any time.
Mzee September 7, 2025
Share this Article
Facebook Twitter Copy Link Print
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

LiwalonaliweLiwalonaliwe
Follow US

© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

[mc4wp_form]
Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Register Lost your password?