Pasua jipu puuuu!-Ngara
Kuna malalamiko ya Vijana Wilaya ya Ngara kupitia taarifa ya kija a mmoja mzalendo aliyejitambulisha kwa ji a la Thitho Philemon kuhusu Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Kanali Mathias Kahabi, kuingilia masuala ya kisiasa kwa kushinikiza upande mmoja na kudhoofisha uhuru wa vijana wenye nia ya kugombea nafasi za uongozi kama Ubunge na Udiwani.
Naweza kusema hili ni joto linaloendelea kupanda kuelekea Uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu 2025. Fomu zitaanza kuchukuliwa June 28 ambapo Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na miongozo ya utumishi wa umma:
Mkuu wa Wilaya ni mtumishi wa umma na mteule wa Rais, hivyo anatakiwa kuwa msimamizi wa serikali katika wilaya bila upendeleo wa kisiasa.
Kuonyesha upendeleo au kuingilia mchakato wa kisiasa kwa kutishia au kudhoofisha wagombea wa upande wowote ni kinyume cha maadili ya utumishi wa umma na pia ni kosa kisheria.
Kauli ya kuwakamata vijana kwa sababu ya kuchukua fomu za kugombea si tu inakiuka haki za msingi za kisiasa na kidemokrasia, bali pia ni matumizi mabaya ya madaraka.
Ikiwa taarifa hii ni sahihi, ni vyema mamlaka husika kama Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, na hata Vyombo vya Dola kupitia Idara ya Usalama wa Ndani kuchukua hatua stahiki za uchunguzi na ufuatiliaji.
Kwakuwa pia yeye ndiye mwenyekiti wa kamati ulimzi na usalama, na mlezi wa makundi yote naweza kusema kweli amechemka na anatakiwa kuomba radhi. Kama haimhusu ajitokeze aweke wazi, ila kama aliteleza pia ajitokeze na kuweka wazi taarifa aeleweke.