Tusidanganyane, Tanzania kuna Amani, ama kuna uoga?
Siku si nyingi tulisikia kuna watu walichukuliwa majumbani, jumba za ibada, kutoka kwenye vyombo vya usafiri na baadae miili yao iliokotwa imeshapoteza uhai.
Inasikitisha baadhi ya watu wanaopotea wanachukuliwa na polisi. Halafu watanzania ambiwa kuwa ndugu zao wapo salama ila ukimya unapovamiwa na jamii, basi polisi hao hao wanakili kuokota miili inayofanana na ndugu waliopotea ama waliochukuliwa na polisi.
Sasa kama chombo cha polis kimegeuka kuwa chombo cha watoa roho, si ingekua vizuri kuwekwa wazi kuwa kazi ya kulinda raia na mali zao wanaitimiza. Ila swala la kulinda uhai halipo kwenye makubaliano.
Ama Chadema peke yao ndio huchukuliwa na kupotezwa? Ikumbuke kina Romani Mkatoliki, Mohamed Dewji walikua sio wana Chadema.
Tuseme watanzania hawawezi kuhimili kuambiwa ukweli ama matusi yanawaumiza? Mo alikua anamtukuna nani, lakini kwani tunaweza sema wengine kupitia nyimbo zao ama kazi zao wanajikuta wanakosoa serikali. Ila serikali kama ni yao, wana haki zote za kuikosoa. Serikali ni sawa na nyumba, unapohisi inavuja, si unachukua muda kutafuta inapovuja ili upazibe? Ukosoaji ni moja ya njia ya kutafuta walipotoboka ili pashughulikiwe.

Ni wangapi wameshapotelea kwenye mikono ya polis?
Mdude,….