Hiki kinachoitwa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kitu gani? Kina manufaa gani kwa mtu wa kawaida kama ukazi tuu katika nchi shirika ni changamoto? Mkenya anaambiwa amevunja sheria anapoishi Tanzania kwa zaidi ya miezi mitatu bila kibali?
Kama mrundi hawezi kuhama na gari lake Rwanda bila kulipa hela ya kodi?
Kama nchi moja inaweza kuvamia nchi nyingine ndani ya jumuia na nchi nyingine kugeuka bubu bila kujaribu kusuruhisha?
Kweli tunahitaji huu muungano ama ni jinsi ya kutengeneza kazi kwa wawakilishi wanaong’aa kwenye suti na luninga?
Tutafakari na tuungane kama kweli dhamira ni kuungana. Kama ni njia ya kutafuna pesa na kuabishana kwani nchi moja inapovamiwa na nyingine, nchi nyingine zinageuka bubu ama chochozi ili ugomvi uendelee.
Hatuwezi kuwa wamoja kama tutaendelea kuwa wanafiki.