Kila siku tunaambiwa serikali haipendi Wafanyakazi na Wananchi wake wakamuliwe na mikopo ya kausha damu. Hivi wanamaanisha au wanatutania ?
Ulishatafakari? Mtu akifungua ofisi za kampuni ya kausha damu tu kinachofuatia ni kuitisha kikao cha siri serious cha kikazi kwenye mgahawa na Mkurugenzi, wakuu wa idara na maafisa utumishi. Mwisho wa utambulishano, kwa posho ya Tsh. 1 – 2 M hao wanaondoka kwenda kuwabadilishia / hamisha vituo vya kazi watumishi 200 – 300 ndani ya halmashauri bila kuwalipa fedha au stahiki za Uhamisho.
Wakiuliza utaskia, “jaza fomu za madai… ila fanya ufanyavyo uhame”.
Kwa kifupi mtu anakopa TSh. 2M za kausha damu ili ajihamishe. Riba ni 30 -50% kwa mwezi
Hebu tafakari maisha ya baadae ya mwalimu au muuguzi aliyekopeshwa TSH. 1.5 au 2M kisha akalipa laki 4 mwezi unaofuatia ukizingatia kwamba riba Mayo pia inazaa.
Miaka miwili baadae unakutana na baadhi ya hao watumishi akili zimefyatuka wanaongea pekee zao mabarabarani deni lishatuna kadiria 30M !
Tulizuieje hili janga na nani alaumiwe ?